Mbabe wa vita mbioni nchini Somalia

10 walifariki katika mapigano yaliyozuka baada ya wanajeshi kushambulia makazi ya Dai
Mapiganao makali yamezuka katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
Vikosi vya serikali vinasema kuwa vimeiteka nyumba hiyo ya Ahmed Dai katika oparesheni iliochukua zaidi ya saa tano.
Ahmed Dai alifanikiwa kutoroka,lakini wapiganaji kadhaa wa kundi lake walikamatwa na silaha zao kuchukuliwa.
Ameambia BBC kwamba ametoroka baada ya wanajeshi wa serikali kuanzisha operesheni kali dhidi yake na wapiganaji wake.
Ahmed Dai huongoza kikosi kikubwa cha wpaiganaji ambao muda wote hutoa ulinzi wa wageni.
Hata hivyo amesema kuwa ataendelea kupigana na kwamba alitumia silaha hizo kujilinda.
Wapiganaji wake walikuwa wakitekeleza oparesheni zao karibu na eneo la uwanja wa ndege linalolindwa sana.
Oparesheni hiyo ya kuwapokonya wapiganaji silkaha ilianza wiki iliopita na serikali inasema kuwa imefanikiwa kupata bunduki 500 pamoja risasi.
Takwimu zinasema kuwa kuna zaidi ya bunduki nusu millioni katika mikono ya raia nchini somali ambako ssheria hazifuatwi
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.