Al-Shabab wateka kambi ya AU Somalia




Wapiganaji wa Al-Shabab wamesema waliua wanajeshi wengi wa Kenya baada ya kuvamia kambi ya majeshi ya Muungano wa Afrika kusini mwa Somalia.
Kundi hilo la Kiislamu limesema limeteka na kudhibiti kambi hiyo mjini el-Ade na kuua wanajeshi 63 wa Kenya.
Wakazi wameambia BBC kwamba wapiganaji hao wa al-Shabab wamepandisha bendera yao katika kambi hiyo na kwamba walionyesha miili ya wanajeshi waliouawa katika barabara za mji huo.
Lakini msemaji wa majeshi ya Kenya Kanali David Obonyo amesema kambi iliyoshambuliwa si ya majeshi ya Kenya.
Badala yake, anasema kambi iliyo karibu ya wanajeshi wa Somalia ndiyo iliyovamiwa na majeshi ya Kenya yalijibu shambulio hilo.
Idadi ya waliofariki kutoka pande zote mbili bado haijabainika, Kanali Obonyo amesema kupitia taarifa.
Ameambia BBC kwamba ripoti kuwa wanajeshi wengi wameuawa ni “propaganda ya kawaida kutoka kwa al-Shabab”.



Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Karibu tena..wasiliana nasi kwa simu namba 0758059936

Chapisha Maoni

 
Top