Kiongozi wa Al Shabaab ashambuliwa

 2 Septemba, 2014 - Saa 14:26 GMT

Haijulikani ikiwa Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo
Wanajeshi wa Mreakani wamefanya mashambulizi ya angani dhidi ya msafara wa magari ya mmoja wa viongozi wa kundi la Al Shabaab nchini Somalia.

Haijulikani ikiwa kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo lililofanyika umbali wa kilomita 240 kusini ya mjini mkuu Mogadishu.

Mwandishi wa BBC anasema kuwa wanajeshi wa Marekani walionekana wakishuka katika eneo hilo kwa helikopta na kuchukua miili ya wapiganaji waliouawa.

Msemaji wa idara ya ulinzi ya Marekani, (Rear Admiral John Kirby) alisema bado inadurusu matokeo ya shambulizi hilo.

Baadhi ya taarifa zinasema kuwa wapiganaji waliwakamata wakazi walioshukiwa kutoa taarifa kwa Marekani.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Karibu tena..wasiliana nasi kwa simu namba 0758059936

Chapisha Maoni

 
Top