Polisi wakana mauaji ya wakazi Tanzania


Media Player

Unahitaji toleo sahihi la Flash Player kucheza sauti/video
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limekanusha madai ya ukiukaji haki za binadamu pamoja na mauaji dhidi ya wakazi wa eneo la Nyamongo linalozunguka mgodi wa machimbo ya dhahabu wa North Mara ulioko Wilayani Tarime mkoani Mara.
Katika Ripoti iliyotolewa hivi karibuni kwenye Bunge la Uingereza na Wanaharakati wa masuala ya madini, polisi kwa kushirikiana na kampuni ya African Barrick inayomiliki mgodi wa North Mara walishutumiwa kwa vitendo vya mauaji na ukatili dhidi ya wananchi waishio jirani na mgodi huo.
Erick David Nampesya alitembelea eneo la Nyamongo kwenye mgodi huo.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Karibu tena..wasiliana nasi kwa simu namba 0758059936

Chapisha Maoni

 
Top